728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, August 12, 2016

    PSG YAANZA MSIMU MPYA UFARANSA KWA USHINDI


    Bastia,Ufaransa.

    MABINGWA wa Ufaransa,Paris Saint-Germain,wameanza vyema kuutetea ubingwa wao baada ya leo usiku kuichapa timu ngumu ya Bastia kwa bao 1-0 katika mchezo mkali na mgumu uliochezwa huko Coriscan,Bastia.

    Bao pekee la mchezo huo limefungwa dakika ya 73 kwa mkwaju mkali na beki wa kushoto Layvin Kurzawa baada ya kipa wa Bastia,Jean-Louis Leca,kuutema mkwaju wa Jese Rodriguez.

    Katika mchezo mwingine uliochezwa usiku huu Monaco na Guingap zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya kufungana mabao 2-2.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PSG YAANZA MSIMU MPYA UFARANSA KWA USHINDI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top