728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, July 19, 2016

    MFUNGAJI BORA ZIMBABWE ATUA AZAM FC

    Dar es Salaam,Tanzania.

    NYOTA wa Kimataifa ya Zimbabwe,Bruce Kangwa, ametua nchini jioni ya
    leo tayari kabisa kufanya majaribio ya kujiunga na Klabu Bingwa ya Afrika
    Mashariki na Kati Azam FC.

    Kangwa anatokea kwa vinara wa Ligi Kuu nchini humo Highlanders FC na
    mpaka sasa ligi hiyo ikiwa
    mapumzikoni kufuatia kumaliza mzunguko wa kwanza, amefanikiwa
    kuwa kileleni kwa ufungaji bora akiwa na mabao saba.

    Mzimbabwe huyo ameshachezea timu
    yake ya Taifa mechi 20 na mpaka sasa yupo kwenye kikosi hicho na anamudu kucheza nafasi tatu tofauti
    uwanjani, beki wa kushoto, winga wa kushoto na mshambuliaji.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MFUNGAJI BORA ZIMBABWE ATUA AZAM FC Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top