728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, May 18, 2017

    Ligi kuu Sauzi nayo yapata bingwa mpya


    Johanesburg,Afrika Kusini.

    Bidvest Wits ama The Clever Boys ndiyo mabingwa wapya wa ligi kuu ya soka nchini Afrika Kusini maarufu kama PSL kwa msimu wa 2016/17 kufuatia ushindi wao wa mabao 2-0 walioupata nyumbani Bidvest Stadium dhidi ya wageni wao Polokwane City.

    Mabao yaliyoandikisha ubingwa huo wa kwanza kwa timu hiyo yamefungwa na James Keene na Daine Klate na kuwaacha kwenye mataa wabingwa wa msimu uliopita Mamelodi Sundowns kwa tofauti ya pointi sita.

    Bidvest Wits inakuwa timu ya saba kutwaa ubingwa wa PSL huku kocha wake,Gavin Hunt akiwa ubingwa huo kwa mara ya nne.Mara tatu akiwa na SuperSport United msimu wa 2007/08, 2008/09 na 2009/10. 


    Matokeo Mengine ya Mei 17 

    Bidvest Wits 2-0 Polokwane City
    Mamelodi Sundowns 2-2 Maritzburg United
    Chippa United 3-0 SuperSport United
    Platinum Stars 2-0 Kaizer Chiefs
    Orlando Pirates 0-0 Ajax Cape Town
    Cape Town City 1-0 Golden Arrows
    Baroka FC 0-0 Highlands Park
    Bloemfontein Celtic 0-0 Free State Stars

    Ligi kuu ya soka nchini Afrika Kusini itafikia tamati Jumamosi Mei 27.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Ligi kuu Sauzi nayo yapata bingwa mpya Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top