728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, May 15, 2017

    Akina Samatta wavuna ushindi ugenini kusaka tiketi ya kucheza Europa Ligi


    Mouscron,Ubelgiji.

    KRC Genk ya Mtanzania,Mbwana Ally Samatta imeendelea kujikusanyia pointi za kutosha kwenye kundi lake la A baada ya usiku wa kuamkia leo ikiwa ugenini kuwatwanga wenyeji wao Royal Excel Mouscron mabao 2-0 huko Stade Le Canonnier ikiwa ni katika muendelezo wa michezo ya kuwania tiketi ya kucheza michuano ya Europa Ligi msimu ujao.

    Katika mchezo huo ulioshuhudiwa Samatta akicheza dakika zote tisini,Genk ilijipatia mabao yote mawili katika kipindi cha pili kupitia kwa Ruslan Malinovsky aliyefunga bao la kwanza katika dakika ya 63 na Jean-Paul Boëtius aliyefunga bao la pili katika dakika ya 70.

    Ushindi huo umeifanya Genk iendelee kujitanua kileleni mwa kundi A baada ya kuvuna pointi 22 katika michezo yake minane.Royal Excel Mouscron iko nafasi ya sita ikiwa na pointi nane baada ya michezo minane.Genk tayari imeshafuzu Europa Ligi.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Akina Samatta wavuna ushindi ugenini kusaka tiketi ya kucheza Europa Ligi Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top