728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, April 04, 2017

    Mtibwa Sugar na biashara isiyo na hasara



    Fadhili Omary Sizya,Morogoro.

    Waswahili husema biashara asubuhi, jioni mahesabu hata wengine huongeza kuwa kile unachokipanda ndicho unachokivuna kuhusu maisha wapo wanaonadi usione mafanikio yanapatikana tambua kuwa mchumia juani hulia kivulini.

    Yote hayo ni maneno ambayo yana maana kubwa sana katika mzungunguko wa kila siku kwenye maisha ya mwanadamu mpaka pale nafsi inafikwa na umauti, duniani watu wanakuja kutafuta ,kila aliyewekeza anajenga jeuri ya alichopandikiza.

    Zunguka kila pande za dunia ukitazama sekta ya michezo kila mmoja amewekeza katika aina tofauti tofauti ambayo huamini hapo ndipo mafanikio yanapo patikana, wapo wafanyabiashara wakubwa kwa upande wa mchezo wa soka ambao huamua kuinyanyua timu kwa kuwekeza kupitia kufanya usajili mkubwa na huamini wanapopata medali za ubingwa,kiasi kikubwa cha mashabiki ambao wataingia uwanjani ikiwemo uuzwaji mkubwa wa tiketi, bidhaa za klabu husika zikifanya vizuri sokoni au wamiliki wao binafsi hufikiri kuhusu kujitengenezea soko ikiwa timu wanazoziendesha zinafanya vizuri, hizo ni baadhi ya chaguzi za kufanya biashara kwa wamiliki wa timu.

    Tukirudi katika ardhi ya nyumbani Tanzania,ukihoji kuhusu chuo au timu iliyomaarufu kufanya biashara ya wachezaji utaambiwa moja kwa moja elekea kanda ya Mashariki mkoani Morogoro, funga safari mpaka wilaya ya Mvomero, kata ya Turiani mtaa wa madizini utafikishwa katika kiwanda cha Sukari ndani ya Mashamba makubwa ya Miwa utaikuta timu inaitwa Mtibwa Suger.

    Ni maarufu watu wa mkoa wa Morogoro hujivunia matunda yanayolelewa huko na baadaye hao vijana kuwika ndani na nje ya nchi, mfano ukisikia majina ya kina Nizar Klalfan alicheza yanga, Vancouver Whitecaps ya Canada,nae Mussa Mgosi kwa sasa meneja wa Simba,Shiza Kichuya mfungaji mahiri wa kona na mipira iliyokufa pale Simba Sc, Salum Mayanga kocha mkuu wa Taifa Stars, Meck Meksime kocha mkuu Kagera Suger ni baadhi ya mafanikio ya kujivunia waliyonayo Mtibwa Suger katika soka nchini hapa.

    Wakiwa wanatengeneza vipaji hivyo, bado Mtibwa sio wazembe katika kupambana kubaki ligi kuu Tanzania, wanaingia katika historia ya kuwa timu iliyokaa muda mrefu katika michuano hiyo, tangu wapande mwaka 1996 ilipokuwa ilikiitwa ligi daraja la kwanza hawakuwahi kushuka daraja mpaka sasa wakiwa na mafanikio ya kutwaa ubingwa mara mbili mfululizo 1999 na mwaka 2000 wakiwa chini ya mwalimu John Simkoko na waliwahi kuubeba ubingwa wa Tusker mwaka 2008.
    Muda wowote kwa sasa ukifika katika kambi ya timu hiyo wapo wachezaji ambao wapo sokoni, wanafanya vizuri kwa kila mechi ikiwa  ligi  inaelekea ukingoni.


    Shaban Nditi

    Tangu ametua kipindi Mtibwa ipo chini ya kocha mkongwe John Simkoko ilikuwa mwaka 2000 akitokea mkoani Singida na alifika hapo kufanya majaribio amedumu mpaka sasa akiwa ni nahodha wa timu hiyo, amekuwa ni kiungo hodari sana, anasifika kwa nidhamu,kiongozi uwanjani yupo tofauti na wachezaji wengi uwanjani akibebwa na uwezo wa kuijua miiko ya soka.

    Nditi ni tegemezi katika klabu hiyo kwa takribani misimu yote aliwahi kutamba akiwa na Marcio Maximo katika timu ya taifa kwa kipindi chote tangu mbrazili huyo alipoteuliwa kuinoa timu hiyo, hachuji uwanjani, burudani ukimtazama anavyotimiza majukumu yake mara zote amekuwa akiwashinda uwezo wa kulimiliki dimba wachezaji wengi wa timu za ligi kuu Tanzania.


    Salim Mbonde

    Yupo klabuni hapo msimu wa tano sasa ,amekuwa beki kisiki anategemewa sana kwa utulivu wake katika eneo la ulinzi, ambapo takribani misimu kadhaa amekuwa akihusishwa kutua katika vilabu vikubwa Tanzania vikiwemo Simba, Azam na Yanga.

    Amekuwa na muendelezo wa kuitwa timu ya taifa na makocha kwa mihula yote ambao hufundisha Taifa Stars, sasa hivi chini ya Salum Mayanga bado anatumainiwa akipendwa zaidi kwa uwezo wa kulinda kiwango chake kwa muda wote.


    Said Mohammedi “Nduda”

    Aliachwa Yanga baada ya kushindwa kutamba kikosi cha kwanza, aliandamwa na majeraha kwa misimu kadhaa, aliwika ligi kuu akitokea Majimaji ya mkoani Songea.

    Sasa hivi panga pangua lazima umkute kikosi cha kwanza labda awe na majeraha ndiyo atakosekana, amejumuishwa Taifa Stars,  amekuwa mlinda mlango anayewanyima magoli wachezaji wengi katika michuano ya ligi kuu, umbo lake zuri la kusimama kulinda nyavu zake, uwezo wa kuelekeza mabeki wake jinsi ya kujipanga hakika amekuwa kipa mwenye uwezo wa juu klabuni hapo.


    Ally Shomary “Alves”

    -Anaweza asiwe na mambo mengi hivyo nadra kufahamika kwa haraka akiwa yupo uwanjani, amedumu klabuni hapo kwa miaka minne sasa akicheza fullbeki ya kulia amekuwa imara kwa misimu yote anayotumika klabuni hapo.

    Aliwahi kuhitajika na Simba Sc, ukimuona anavyocheza utagundua ni hodari kuimudu nafasi yake, anapanda kwa haraka na kurudi kukaba kwa kasi hiyo hiyo, makocha waliopita kwa kipindi tofauti klabuni hapo akina Mecky Mekxime, Salum Mayanga na sasa hivi ikinolewa na Zuberi Katwila mara zote hawana chaguo zaidi ya Ally Shomary.


    Mohammed Issa “Mo Banka”

    -Huu ni msimu wake wa kwanza akiwa na Mtibwa Suger akitokea visiwani Zanzibar, lakini ukimtazama anavyolivuruga dimba,akiteleza kama kambale ni kama amecheza misimu mingi ligi kuu bara au amekaa kikosini hapo kwa muda mrefu.

    Amekuja klabuni hapo kwa kazi mojatu ! ambayo ni kuziba nafasi walizokuwa wakicheza Mohammed Ibrahim na Mzamiru Yassin waliouzwa Simba Sc, sasa akisaidiana na kina Ibrahim Jeba, Shaban Nditi amekuwa moto wa kuotea mbali kwa viungo wengi ligi kuu Bara.


    Japhar Salum

    Umri wake hauwezi kuzidi miaka 22, ametokea Mtibwa B anamudu vizuri safu ya ushambuliaji akisimama katikati, binafsi akiwa na nguvu za kutosha kumiliki mpira lakini anatisha sana baada ya kuwa na watu wanaomlisha vya kutosha nao wakiwa na kash kasha kina Stamil Mbonde, Said Bahanuz na hata akipangiwa kucheza na machachari Vicent Barnabas amekuwa hatari sana anapolitizama lango la timu pinzani.

    Sasa hivi amekuwa na manufaa zaidi akiwa na uwezo wa kupiga mipira ya adhabu, akimudu kuibeba mtibwa tangu mfungaji wao Rashid Mandawa mwenye mabao 7 akumbwe na majeraha, kijana huyo ameendelea kuonyesha makali zaidi katika safu ya Ushambuliaji.







    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Mtibwa Sugar na biashara isiyo na hasara Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top