Dortmund,Ujerumani.
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Gabon,Pierre-Emerick Aubameyang hatajiunga na vilabu vingine vya barani Ulaya katika dirisha lijalo la usajili zaidi ya Real Madrid na Barcelona.Hii ni kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa klabu yake ya Borussia Dortmund,Hans-Joachim Watzke.
Watzke ametoa kauli hiyo baada ya hivi karibuni Aubameyang mwenye umri wa miaka 27 kuripotiwa kuwa kwenye mawindo ya vilabu mbalimbali vikubwa barani humo vikiwemo vilabu tajiri vya nchini England vya Manchester City,Liverpool na Arsenal.
Watzke anaamini kuwa Real Madrid na Barcelona ndivyo vilabu pekee vyenye hadhi ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Saint Etienne ya Ufaransa na kusisitiza kuwa angependa kumwona Aubameyang akijiunga navyo siku moja.
Aidha Watze ameongeza kuwa mshambuliaji huyo anayekadiriwa kuwa na thamani ya £100m hata iweje hatauzwa kwenda kwa mahasimu wao wakubwa wa Bundesliga,Bayern Munich kama ilivyokuwa kwa Wajerumani Mario Gotze na Mats Hummels waliouzwa kwenda Allianz Arena katika vipindi viwili tofauti. Aubameyang bado ana mkataba na Borussia Dortmund mpaka mwaka 2020.
0 comments:
Post a Comment