728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, July 12, 2016

    WAMISRI KUCHEZESHA YANGA,MEDEAMA JUMAMOSI

    Cairo,Misri.

    Waamuzi kutoka Misri ndiyo watakaochezesha mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya Yanga
    na Medeama ya Ghana itakayochezwa Julai 16 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

    Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua Ibrahim Nour El Din kuwa mwamuzi wa kati kwenye mechi hiyo wakati waamuzi wasaidizi ni Ayman Degaish na Samir Gamal Saad.

    Mohamed Maarouf Eid Mansour atakuwa mwamuzi wa akiba. Waamuzi wote ni raia wa Misri.

    Raia wa Zambia,Pasipononga Liwewe
    atasimama kama kamisaa, Mfubusa Bernard kutoka Burundi atakuja kama mkaguzi wa waamuzi huku Ian Peter Keith Mc Leod kutoka Afrika Kusini ndiye mratibu mkuu wa pambano.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WAMISRI KUCHEZESHA YANGA,MEDEAMA JUMAMOSI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top