728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, July 04, 2016

    UFARANSA YAIFANYIA MAUAJI ICELAND NA KUIFUATA UJERUMANI NUSU FAINALI ULAYA

    Ufaransa.

    IKICHEZA soka la kuvutia na la ufundi wa hali ya juu, timu ya taifa ya Ufaransa,imetinga nusu fainali ya michuano ya Euro 2016 baada ya usiku huu kuifumua Iceland kwa mabao 5-2 katika mchezo mkali wa robo fainali uliochezwa katika uwanja wa Stade de France,Paris.

    Mpaka mapumziko, Ufaransa ilikuwa kifua mbele kwa mabao manne ya Olivier Giroud,Paulo Pogba,Dimitri Payet na Antoine Griezman.

    Mwanzoni mwa Kipindi cha pili,Olivier Giroud aliifungia Ufaransa bao la tano kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na Dimitri Payet.Mabao ya Iceland yamefungwa na Kolbeinn Sigthórsson pamoja na Birkir Bjarnason.

    Kwa kushinda mchezo huo,Ufaransa sasa itavaana na Ujerumani katika mchezo wa nusu fainali utakaochezwa Alhamis.Hii ni nusu fainali yake ya kwanza tangu mwaka 2000.

    Ujerumani ilitinga nusu fainali baada ya kuifunga Italia kwa penati 6-5 kufuatia sare ya bao 1-1 ndani ya dakika 120.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: UFARANSA YAIFANYIA MAUAJI ICELAND NA KUIFUATA UJERUMANI NUSU FAINALI ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top