728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, July 08, 2016

    DANNY MRWANDA ASAINI KAGERA SUGAR

    Kagera,Tanzania.

    MSHAMBULIAJI wa zamani wa Majimaji,Danny Mrwanda, amesaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuitumia Kagera Sugar kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

    Mrwanda aliwahi kuzichezea Simba, Polisi Moro, Yanga katika misimu tofauti kabla ya kusajiliwa na Majimaji katika dirisha dogo la Ligi Kuu Bara msimu uliopita.

    Akithibitisha usajili huo,Mratibu wa Kagera Sugar, Mwinyi Mwinyi,amesema wamewasainisha mkataba wa mwaka mmoja Mrwanda na mchezaji mwenzake, Japhet Vedastus kutoka Toto Africans.

    Mwinyi alisema usajili huo umetoka na mapendekezo yaliyotolewa na Kocha wao Mkuu,Adolf Richard kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao tayari kwa msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom
    Tanzania Bara.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: DANNY MRWANDA ASAINI KAGERA SUGAR Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top