728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, September 12, 2015

    EPL:ARSENAL MWENDO MDUNDO YAIFUMIA STOKE CITY EMIRATES,MNIGERIA AIBEBA MAN CITY

    London,England.

    Arsenal imeibuka na ushindi wa kwanza nyumbani baada ya kuifunga Stoke City kwa mabao 2-0 katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa jioni ya leo katika dimba la Emirates.

    Arsenal imepata magoli yake kupitia kwa Theo Wallcot alifunga dakika ya 31 akimalizia pasi nzuri ya Mesut Ozil.Goli la pili la Arsenal limefungwa na Oliver Giroud kwa kichwa dakika ya 85 akiunganisha mpira wa wa Santiago Cazorla.

    Kwingineko Manchester City imeendeleza wimbi lake la ushindi baada ya kuifunga Crystal Palace kwa goli 1-0.Goli la Manchester City limefungwa na kinda Mnigeria Kelechi Iheanacho

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: EPL:ARSENAL MWENDO MDUNDO YAIFUMIA STOKE CITY EMIRATES,MNIGERIA AIBEBA MAN CITY Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top