Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho amemtoa kafara daktari wa timu hiyo, Eva Carneiro, akidai kwamba alichangia kwenda kwao sare 2-2 na Swansea wikiendi iliyopita, ambapo amemwondosha kwenye benchi lake.
Japokuwa Mourinho alionesha wazi kukasirishwa na hatua ya Carneiro kwenda kumtibu Eden Hazard kwa kitambo wakati Chelsea wakiwa tayari wamempoteza kwa kadi nyekundu kipa wa Thibaut Courtois, ukweli ni kwamba daktari huyo aliitwa uwanjani na mwamuzi Michael Oliver.
Mourinho amemshusha cheo daktari huyo mwenye mvuto miongoni mwa washabiki wa Chelsea lakini sasa Mourinho ameamua kumvua kazi zake za kuwatibu wachezaji wa kikosi cha kwanza kwenye mechi. Carneiro aliitwa uwanjani mara mbili na mwamuzi Jumamosi hii.
Jumanne hii, mwanamama huyo ameelezwa kwamba hatakaa tena kwenye benchi la matabibu wa timu hiyo. Hazard alianguka baada ya kukabiliana na mchezaji wa Swansea, Gylfi Sigurdsson.
Picha ya video inaonesha wazi mwamuzi akiwaita mara mbili matabibu hao na laiti Carneiro angetumia kama utetezi huenda angerejeshewa majukumu yake.
0 comments:
Post a Comment