728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, August 18, 2015

    SIMBA UBABE,YANGA UBABE,AZAM NAYO UBABE LIGI KUU BARA


    YANGA, Azam na Simba, zimezidi kutunishiana misuli kila moja ikitamba kufunika msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara kutokana na madai ya kuwa na kikosi bora baada ya usajili wa dirisha linalotarajiwa kufungwa keshokutwa.


    Yanga ambao ndio mabingwa wa Tanzania Bara, wamekuwa wakijifua kwa takribani miezi miwili sasa kama ilivyokuwa kwa Azam, huku timu hizo zikiwa zimeongeza nguvu katika vikosi vyao kwa kusajili wachezaji wapya, wazawa na wa kigeni kama ilivyo kwa Simba.



    Kati ya wachezaji wanaowapa jeuri Yanga, ni kiungo mshambuliaji mpya, Geoffrey Mwashiuya iliyomsajili kutoka Kimondo FC ya Mbozi, Mbeya, Malimi Busungu (Mgambo Shooting), Deus Kaseke (Mbeya City), Haji Mwinyi, Matheo Simon na kipa Mudathir Khamis (KMKM) ambao waling’ara vilivyo na timu hiyo kwenye michuano ya Kombe la Kagame iliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam na mechi kadhaa za kirafiki.



    Pia wapo wachezaji wa kigeni kama mshambuliaji,Donald Ngoma nakiungo, Thaban Kamusoko kutoka Zimbabwe na beki wa kati, Vincent Bossou raia wa Togo.



    Wachezaji hao wapya na wale wa zamani kama viungo Haruna Niyonzima, Salum Telela, Ally Mustapha ‘Barthez’, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kelvin Yondani, Andrey Coutinho, Simon Msuva na wengineo ndio wanaoonekana kumpa jeuri Kocha Mkuu wao, Mholanzi Hans van der Pluijm ambaye ameweka wazi kuwa msimu ujao ni wao.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SIMBA UBABE,YANGA UBABE,AZAM NAYO UBABE LIGI KUU BARA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top