728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, August 14, 2016

    MAN UNITED YAICHAPA BOURNEMOUTH NA KUKAA KILELENI ENGLAND



    Bournemouth,England.

    JOSE Mourinho amekianza vyema kibarua chake cha kuinoa Manchester United baada ya mchana huu kukiongoza kikosi chake kuichapa AFC Bournemouth kwa mabao 3-1 katika mchezo mkali wa ligi kuu England uliochezwa katika uwanja wa Vitality Stadium.

    Katika mchezo huo uliochezeshwa na Mwamuzi,Andre Marriner,Manchester United imejipatia mabao hayo kupitia kwa Juan Mata 40',Wayne Rooney 58 na Zlatan Ibrahimovic 64' bao la AFC Bournemouth limefungwa na Mlinzi,Adam Smith 69'

    Matokeo hayo yameifanya Manchester United kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi kuu England kwani hakuna timu yoyote ambayo mpaka sasa imefunga mabao matatu.






    Takwimu

    Umiliki (Possesion):Manchester United imemiliki mchezo kwa asilimia 53,Bournemouth 47.

    Mchezaji Bora wa Mechi:Wayne Rooney

    Vikosi.

    Bournemouth XI: Boruc,Francis, Adam Smith, Steve Cook,Daniels, Ibe, Surman, Arter, Lewis Cook,Wilson, King 

    Manchester United XI: De Gea,Valencia, Bailly, Blind, Shaw, Fellaini,Herrera, Mata, Rooney, Martial,Ibrahimovic


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAN UNITED YAICHAPA BOURNEMOUTH NA KUKAA KILELENI ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top