728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, July 18, 2016

    TP MAZEMBE,MO BEJAIA ZASHINDWA KUTAMBIANA SHIRIKISHO

    Mashabiki wa TP Mazembe 

    Bejaia,Algeria.

    TP Mazembe na Mo Bejaia zimechoshana nguvu baada ya kutoka sare ya bila kufungana katika mchezo mkali wa Kundi A wa Kombe la Shirikisho Afrika uliochezwa Usiku huu katika Uwanja wa Stade de l'UnitƩ MaghrƩbine,huko Bejaia-Algeria.

    Kwa matokeo hayo TP Mazembe inaendelea kuongoza Kundi A baada ya kufikusanyia pointi saba kufuatia kushuka dimbani mara tatu.Mo Bejaia ni ya pili ikiwa imejikusanyia pointi tano,Medeama FC ni ya tatu ikiwa na pointi mbili huku Yanga SC ikiwa mkiani na pointi yake moja.Timu zote zimecheza michezo mitatu mitatu.

    Michezo ya marudiano ya kundi A inatarajiwa kufanyika Julai 27 ambapo TP Mazembe watakuwa wenyeji wa MO BĆ©jaĆÆa huko Stade TP Mazembe,Lubumbashi,Congo DR.Yanga watasafiri mpaka Sekondi-Tokoradi,Ghana kuvaana na Medeama FC 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TP MAZEMBE,MO BEJAIA ZASHINDWA KUTAMBIANA SHIRIKISHO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top