728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, July 09, 2016

    SHIZA KICHUYA RASMI SIMBA SC,MTIBWA KUSAKA MRITHI WAKE WIKI HII

    Turiani,Morogoro.

    KLABU ya Mtibwa Sugar
    imethibitisha kukamilisha dili la kumuuza mchezaji wao Shiza Kichuya kwa klabu ya Simba.

    Kichuya alitajwa kumezewa mate na Simba kwa muda mrefu ambapo Msemaji wa Mtibwa Sugar,Thobias Kifaru amesema kuwa
    tayari wamemalizana na klabu na mchezaji ameshajiunga na wekundu
    hao wa Msimbazi. 

    Alisema mchezaji huyo sasa ni mali ya Simba na kwamba wanaangalia namna ya kuziba pengo lake kwa kufanya usajili mwingine kuanzia wiki ijayo.

    “Tayari tumekamilisha dili la kumuuza Kichuya, kwa hiyo ameshajiunga na wenzake wa Simba, ni mchezaji mzuri
    tunasikitika lakini hatuna jinsi,tutaangalia wengine wa kuziba pengo lake,” alisema. 

    Kusajiliwa kwa Kichuya kutakamilisha jumla ya wachezaji watatu wakitokea Mtibwa Sugar na kuuzwa katika timu hiyo ya Simba.Wengine ni Mohamed Ibrahim na Muzamil Yasin. 


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SHIZA KICHUYA RASMI SIMBA SC,MTIBWA KUSAKA MRITHI WAKE WIKI HII Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top