728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, July 09, 2016

    PAPIS DEMBA CISSE AIHAMA NEWCASTLE UNITED NA KUFUATA MAPESA CHINA

    Shanghai, China.

    MSHAMBULIAJI Mkongwe wa Senegal,Papiss Demba
    Cisse ameihama Newcastle United na kujiunga na Shandong Luneng inayoshiriki ligi kuu ya China kwa ada ya Paundi Milioni 5.

    Cisse,31,alijiunga na Newcastle United mwaka 2012 akitokea Freiburg ya Ujerumani kwa ada ya Paundi Milioni 10 amejiunga na Shandong Luneng mchana huu baada ya kufaulu zoezi la upimaji wa afya.

    Cisse ameiacha Newcstle United akiwa ameifungia mabao 44 katika michezo 131 ya michuano mbalimbali.

    Ligi ya China imegeuka kivutio ndani ya miaka hii miwili kutokana na vilabu vyake kusajili kwa madau makubwa pamoja na kulipa mishahara mizuri hali ambayo imewafanya nyota wengi wa soka kuikimbilia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PAPIS DEMBA CISSE AIHAMA NEWCASTLE UNITED NA KUFUATA MAPESA CHINA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top