728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, October 03, 2015

    HAKUNA NAMNA:CHELSEA YAJIANZAA KUVUNJA BENKI ILI KUMNASA FUNDI HUYU WA KIRENO


    London,England.

    SIYO SIRI TENA.Taarifa za ndani toka klabu ya Chelsea zinadai kuwa kocha mkuu wa miamba hiyo ya ligi kuu ya England,Mreno Jose Mourinho anajiandaa kukipa makali zaidi kikosi chake ifikapo mwezi januari kwa kumsajili kiungo mahiri wa FC Porto Ruben Neves.

    Taarifa zaidi zinadai tayari Chelsea imeshaandaa kitita cha nguvu cha £29m ili kuhakikisha inamnasa nyota huyo mwenye umri wa miaka18 ambaye pia anawindwa kwa karibu na miamba ya Hispania na Ulaya FC Barcelona.

    Chelsea imeongeza kasi katika mbio za kumnasa Neves baada ya kinda huyo kuonyesha kiwango kizuri na kuisaidia FC Porto kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi yao katika mchezo wa ligi ya mabingwa jumanne wa ligi ya mabingwa Ulaya.




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: HAKUNA NAMNA:CHELSEA YAJIANZAA KUVUNJA BENKI ILI KUMNASA FUNDI HUYU WA KIRENO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top