728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, August 10, 2015

    USAJILI ENGLAND WAZIDI KUPAMBA MOTO,WEST BROM YAWEKA REKODI MPYA KATIKA USAJILI YAMWAGA MTONYO MREFU KUSAJILI MSHAMBULIAJI


     Klabu ya West Bromwich Albion imeandika historia mpya katika vitabu vyake vya kumbukumbu baada ya leo hii kukamilisha usajili wa mshambuliaji hatari Salomon Rondon kutoka klabu ya Zenit St Petersburg kwa kitita cha paunti milioni 12.

    Kitita hicho ni kikubwa zaidi kuwahi kutumiwa na klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu nchini Englang.Kabla ya kumsajili Rondon West Brom haikuwahi kutumia kitita kama hicho katika usajili tangu ilipoanzishwa miaka mingi nyuma.

    West Brom imemsajili Rondon kwa ajili ya kuimarisha safu yake ya ushambuliaji ambayo kwa kipindi kirefu imekuwa ikimtegemea zaidi kinda Saido Berahino ambaye kwa kipindi kirefu sana amekuwa akiwindwa na klabu ya Tottenham.

    Rondon mzaliwa wa Venezuela ameiacha Zenit baada ya msimu uliopita kuifungia magoli 16 na kuibuka mfungaji bora katika ngazi ya klabu akimzidi Hulk.Jumla msimu uliopita Rondon alifunga magoli 28 katika michezo 57




    Embedded image permalinkSalomon Rondon scored 16 league goals last season, more than any other Zenit player.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: USAJILI ENGLAND WAZIDI KUPAMBA MOTO,WEST BROM YAWEKA REKODI MPYA KATIKA USAJILI YAMWAGA MTONYO MREFU KUSAJILI MSHAMBULIAJI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top