728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, August 11, 2015

    SUPER CUP:LEO NI FC BARCELONA v FC SEVILLA,FAHAMU MENGI KUHUSU MTANANGE HUO

    Leo ni leo katika dimba la  Boris Paichadze Dinamo Arena,Georgia pale miamba ya La liga FC Barcelona na FC Sevilla itakapovaana kuwania Super Cup ya vilabu bingwa Ulaya.Mtanange huu huwa ni ishara ya ufunguzi wa ligi mbili za bara hili [Europa na Ligi ya mabingwa].

    FC Barcelona inaingia katika mtanange wa leo ikiwa kama bingwa wa ligi ya mabingwa huku FC Sevilla ikiingia kama ligi wa Europa.

    Tadhimini fupi kuelekea mchezo huo;Tangu mwaka 2010 vilabu hivi vimekutana mara 12 na katika mara zote hizo FC Sevilla haijawahi kuibuka mshindi mbele ya FC Barcelona,Je leo itakuwaje?

    UWANJA UTAKAOPIGIWA MTANANGE HUO;9:45 USIKU


    BorisPaichadzeDinamoArena.jpg
     Mchezo huo utapigwa katika dimba hili liitwalo Georgia, Boris Paichadze Dinamo Arena. 
     
    VIKOSI
    Barcelona XI: Ter Stegen; Alves, Pique, Mascherano, Mathieu; Busquets, Rakitic, Iniesta; Pedro, Suarez, Messi.

    Sevilla XI: Rico; Mariano, Coke, Krychowiak, Trémoulinas; Banega, Krohn-Dehli; Reyes, Iborro, Konoplyanka; Gameiro.



    Emery.jpg
                                                       Unai Emery kocha wa Sevilla

     NYOTA WATAKAOKOSA MTANANGE HUO
     
    Neymar,Jordi Alba na Douglas huku Sevilla wao wataikosa huduma ya kiungo Steven Nzonzi anayeumwa tumbo,huku mlinzi Adil Rami na Ciro Immobile wakiwa mguu ndani mguu nje kuwemo katika mtanange huo.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SUPER CUP:LEO NI FC BARCELONA v FC SEVILLA,FAHAMU MENGI KUHUSU MTANANGE HUO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top