Pilika pilika za usajili zimeendelea kushika kasi barani Ulaya kwa wachezaji na makocha kuhama toka kilabu kimoja na kwenda kingine.
Leo klabu ya Stoke City imeendelea kukiimarisha kikosi chake baada ya kuinasa saini ya winga hatari Xherdan Shaqiri,23 toka klabu ya Inter Milan kwa ada ya rekodi ya £12m.Shaqiri amesaini mkataba wa miaka mitano kuichezea Stoke City baada ya mambo kumuendelea kombo Italia.
Klabu ya AC Milan imefanikiwa kumsajili mlinzi Alessio Romagnoli,20 toka AS Roma kwa kitita cha €28m
Baada ya kucheza soka Urusi kwa kipindi cha msimu mmoja tu winga Mathieu Valbuena,30 amerudi nyumbani kwao Ufaransa na kujiunga na klabu ya Olympique Lyonnais kwa kitita cha £3.5m akitokea Dynamo Moscow
0 comments:
Post a Comment