Siku ya jana jumanne klabu ya Stoke City ilipokamilisha usajili wa winga Xherdan Shaqiri kutoka klabu ya Inter Milan ya Italia siyo kwamba ilikuwa ikiandika historia ya matumizi makubwa zaidi ya pesa katika usajili kwa mchezaji mmoja bali pia ilikuwa ikiandika historia nyingine ya kuwa na kikosi kilichojaa wachezaji wengi waliowahi kutwaa ubingwa wa ligi ya mabingwa Ulaya kuliko klabu yoyote ili inayoshiriki ligi kuu nchini England.Shaqiri ametua Stoke City kwa kitita cha paundi milioni 12 kikiwa ni kiwango kikubwa zaidi kutumiwa na klabu hiyo tangu kuanzishwa kwake miaka ya 1860-62.Jumla ya nyota hao ni zaidi
ya idadi ya nyota wote walioko katika vilabu vya Arsenal,Man City na Liverpool wakiwekwa pamoja.
Ifuatayo ni orodha kamili ya vilabu na nyota waliowahi kutwaa ligi ya mabingwa
(1) Stoke City:Marko Arnautovic (Inter 2010), Bojan (Barcelona 2009 na 2011) Marc Muniesa (Barcelona 2009). , Ibrahim Afellay (Barcelona 2011),, Xherdan Shaqiri (Bayern Munich 2013),
(2) Manchester United:Michael Carrick, Wayne Rooney, Victor Valdes, Juan Mata, Bastian Schweinsteiger
(3)Chelsea:John Terry, Gary Cahill, John Obi Mikel, Ramires, Branislav Ivanovic
(4) Liverpool:Mario Balotelli na Danny Sturridge
(5) Arsenal:Peter Cech
Man City:Yaya Toure (Barcelona 2011)
0 comments:
Post a Comment