728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, August 13, 2015

    DZEKO AAHIDI MVUA YA MATAJI AS ROMA

    Roma,Italia.

    Mshambuliaji mpya wa AS Roma Edin Dzeko raia wa Bosnia-Herzegovina ametamba kuipa mataji ya kutosha klabu hiyo kongwe ya Seria A.Dzeko aliyekamilisha usajili wake wa mkopo jana jumatano akitokea Manchester City kwa ada ya euro milioni 4 amesema ametua Roma kurudia kile alichokifanya England katika klabu ya Manchester City.Roma haijatwaa Seria A tangu mwaka 2000-2001.

    Amesema [Nimekuja hapa kuisaidia Roma (Giallorossi) iweze kutwaa mataj,lakini yote haya yatafanikiwa tukiweka bidii uwanjani.]
    Edin Dzeko to Roma: Latest Transfer Details, Reaction and More
    Dzeko akiwa mazoezini AS Roma

     Akiongelea kilichomvutia zaidi Roma...Dzeko amesema [Ushawishi mkubwa umetoka kwa rafiki  yangu Miralem Pjanic ambaye anacheza hapa .Mkurugenzi wa michezo Walter Sabbatini nae amefanya kazi kubwa.Wameniambia mengi mazuri kuhusu hapa hali ya hewa,mji na mshabiki.
    Embedded image permalink
    Jumla ya michezo aliyocheza Dzeko akiwa na Man City

    Dzeko ametua Roma baada ya kuichezea Manchester City jumla ya michezo 185 na kuifungia jumla ya magoli 71 huku mengi akiwa ameyafunga akitokea benchi.Pia ametwaa mataji mawili ya ligi kuu,FA Cup mara moja,Ngao ya jamii mara moja na Capital One Cup mara moja.Roma itamsajili jumla Dzeko msimu ujao kwa ada ya euro milioni 11.

     
    Dzeko akisaini mkataba
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: DZEKO AAHIDI MVUA YA MATAJI AS ROMA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top