728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, August 19, 2016

    SIMBA SC YAPATA ITC YA MAVUGO SASA KAZI MOJA TU


    Dar Es Salaam,Tanzania.

    SASA ni rasmi kuwa Mshambuliaji wa Kimataifa wa Burundi,Laudit Mavugo,ataichezea Simba SC katika michuano ya Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara pamoja na ile ya Kombe la Shirikisho (FA) hii ni baada ya leo mchana klabu hiyo yenye makao yake makuu Msimbazi,Dar Es Salaam kupokea hati yake ya uhamisho wa kimataifa ( ITC ).

    Mbali ya Mavugo mshambuliaji mwingine wa klabu hiyo aliyekuwa na hatihati ya kuikosa michezo ya mwanzo ya Ligi kuu ni Muivory Coast,Frederic Blagnon,lakini nae ITC yake imepatikana.

    Kuwasili kwa hati hizo kunawapa Simba SC uhalali wa kuwatumia wachezaji hao katika michuano yote itakayoihusisha klabu hiyo ambayo msimu huu imepania kutwaa ubingwa wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara 

    Mavugo alisajiliwa na Simba SC hivi karibuni baada ya kumaliza mkataba katika klabu ya Vital’o huku Blagnon akijiunga kutoka kwa miamba ya Ivory Coast,Africa Sports.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SIMBA SC YAPATA ITC YA MAVUGO SASA KAZI MOJA TU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top