728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, August 10, 2015

    YANGA YAIPIGA BAO SIMBA YAMSAJILI STRAIKA WA KMKM ALIYENG'ARA KAGAME




    Dar es salaam,Tanzania.

    Yanga Sc imemnasa mshambuliaji matata wa KMKM ya Zanzibar Matheo Antony Simon.Matheo ambaye alikuwa akipigiwa hesabu pia na klabu ya Simba SC amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuwachezea mabingwa wa Tanzania [Yanga] jana jumapili usiku.

    Matheo alianza kunyatiwa na Simba SC baada ya kung'ara kwenye michuano ya Kagame kabla ya mapema wiki iliyopita kuifunga Simba SC magoli mawili katika mchezo wa kirafiki ambao KMKM ililala kwa bao 3-2.

    Matheo atasafiri leo kuelekea Tukuyu,Mbeya kujiunga na Yanga iliyoweka kambi mkoani humo kwa ajili ya kujiwinda na mchezo wa ngao ya jamii dhidi ya Azam FC Agosti 22.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: YANGA YAIPIGA BAO SIMBA YAMSAJILI STRAIKA WA KMKM ALIYENG'ARA KAGAME Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top