728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, August 02, 2015

    KEANE:ARSENAL WANAPENDA SANA KUUZA SURA KULIKO KUTWAA TAJI LA EPL

    Unamkumbuka Roy Keane yule nahodha wa zamani wa Manchester United?Yule aliyekuwa hapikiki chungu kimoja na nahodha wa zamani wa Arsenal Patrick Vieira?Sasa ameibuka na hili.

    Akifanya mazungumzo na gazeti la Daily Star,Roy Keane amesema Arsenal ina wachezaji wazuri.Wenye tabia nzuri lakini tatizo lao ni kuwa wanapenda sana kujipiga picha "Selfie" kuliko kutwaa taji la ligi kuu (EPL)

    Amesema "Wachezaji wa Arsenal wanapenda selfie,kujenga miili yako ionekane yenye mvuto "six packs" na kuweka mitindo mbalimbali ya nywele lakini linapokuja suala la kutwaa mataji kwao inakuwa ni hadithi tofauti.

    "Kila mwaka sababu zimekuwa ni zile zile.Siku za karibuni Arsenal imejitahidi kununua wachezaji wazuri lakini sidhani kama kuna yeyote anayeweza kupata nafasi katika kikosi cha Chelsea"Alimaliza Roy Keane.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KEANE:ARSENAL WANAPENDA SANA KUUZA SURA KULIKO KUTWAA TAJI LA EPL Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top