728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, August 17, 2015

    SUB YA TERRY YAENDELEA KUWAPASUA VICHWA WACHAMBUZI WA SOKA ENGLAND


    Graeme Souness amepinga mawazo ya mchambuzi mwenzake wa soka anayedai kwamba kitendo cha John Terry kutolewa jana katika mechi dhidi ya Manchester City ni kumtaarifa mmiliki wa klabu hiyo, Roman Abromavic kuwa maisha ya soka ya nahodha huyo yanaelekea ukingoni.

    Kwa mara ya kwanza nafasi ya Terry ilichukuliwa na Kurt Zouma baada ya dakika 45 tu.
    Haijawahi kutokea Kwa Terry kufanyiwa 'sub' katika mechi 177 chini ya kocha Jose Mourinho.
    Akizungumza kwenye uchambuzi wa baada ya mechi wa Sky Sports, Souness, anaamini Terry alitolewa kwasababu tu ya presha ya Mourinho.
    "Nadhani Terry alikuwa bora kuliko Gary Cahill, sikuona kama alicheza vibaya. John Terry ni kiongozi". Alisema Souness.
    "Nadhani kocha anajaribu kumwambia kwa vitendo mmiliki wa timu kwamba anahitaji wachezaji zaidi. Kama stori ni za kweli basi anapenda wachezaji wengi (Mourinho). Nadhani alikuwa anasisitiza hoja hiyo kwa vitendo akimtoa Terry".
    Souness alikuwa anabadilishana mawazo na mchambuzi mwenzake, Niall Quinn, ambaye alidai kwamba kitendo hicho ni dalili ya soka la nyota huyo wa zamani wa England kumalizika.
    Quinn, mchezaji wa zamani wa Manchester City anaamini sasa Terry anakabiliwa na changamoto ya kupigania namba yake katika kikosi cha kwanza.
    "Tuliona picha zake akiwa kwenye benchi baada ya sub, naamini yeye mwenyewe ameshaanza kuwaza kwamba anakwenda kugombania namba kwenye timu".
    "Sidhani kama Terry atacheza wikiendi ijayo (dhidi ya West Brom). Naamini ana kazi kubwa ya kumshawishi kocha wake. Huu unaweza kuwa mwanzo wa kuisha kwa soka lake".
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SUB YA TERRY YAENDELEA KUWAPASUA VICHWA WACHAMBUZI WA SOKA ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top