728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, August 17, 2015

    SERGIO RASMI AJIFUNGA MIAKA MITANO ZAIDI REAL MADRID,AIKANA MANCHESTER UNITED

    Baada ya tetesi nyingi za kuwa anahama na kujiunga na Manchester United hatimaye mlinzi Sergio Ramos ameamua kubaki Real Madrid na leo mchana amesaini mkataba mpya wa miak mitano utakaomuweka Santiago Bernabeu mpaka mwaka 2020.

    Ramos,29  aliyetua Real Madrid mwaka 2005 akitokea Sevilla amesaini mkataba huo mpya mchana wa leo katika uwanja wa Santiago Bernabeu katika sherehe fupi iliyovuta macho ya wengi.Kufuatia mkataba huo mpya Ramos atakuwa akivuna mshahara wa £123,000 kwa wiki baada ya kukatwa kodi.
              Sergio Ramos at Real Madrid
    Akiulizwa kwanini ameamua kubaki Madrid,Ramos amesema "Hakuna klabu kubwa duniani.Furaha yangu ndiyo kipaumbele changu katika maamuzi yoyote yale."Pesa haijabadili akili yangu.Furaha na familia ndiyo kipaumbele changu.Sikuwahi kusema kuwa nataka kuhama Real Madrid."Chochote ambacho vyombo vya habari zinasema naheshimu lakini ukweli wa jambo hili uko tofauti kidogo.

     "Ndoto yangu imekuwa ni kuwa hapa siku zote na ikibidi kustaafia hapa."Kwa kweli,kama lingekuwa ni suala la kiuchumi basi nisingebaki hapa.Halikuwa swala la pesa."Alisisitiza Ramos.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SERGIO RASMI AJIFUNGA MIAKA MITANO ZAIDI REAL MADRID,AIKANA MANCHESTER UNITED Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top