728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, January 29, 2016

    MAMBO YA PESA:WAJUE NYOTA WA LIGI KUU ENGLAND WALIOKWENDA KUVUNA PESA CHINA

    Na Paul Manjale.

    Ukiachana na nchi za Marekani pamoja na Qatar nchi ya China imegeuka kivutio kwa wachezaji wengi wa soka wa Ulaya,Amerika,Afrika na kwingineko.

    Sababu kubwa inayotajwa ni mishahara minono pamoja na posho za kutakata kwani ndani ya miezi 12 tu iliyopita vilabu vya China vimetumia pesa nyingi kunogesha ligi yao kwa kusajili wachezaji wenye majina makubwa duniani.

    Wafuatao ni wachezaji waliojiunga na vilabu vya China baada ya kutesa ligi kuu England huku Ramires akiweka rekodi ya kuwa mchezaji ghari zaidi baada ya mapema wiki hii kujiunga na Jiangsu Suning kwa dau la £25m.

    Ramires - Jiangsu Suning.Amecheza Chelsea

    Paulinho - Guangzhou Evergrande.Amecheza Tottenham

    Demba Ba-Shanghai Shenhua.Amecheza Westham,Newcastle na Chelsea.

    Gervinho -Hebei Fortune FC.Amecheza Arsenal FC

    Asamoah Gyan - Shanghai SIPG.Amecheza Sunderland.

    Tim Cahill - Shanghai Shenhua.Amecheza Everton.


    Mohammed Sissoko - Shanghai Shenhua.Amecheza Liverpool 


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAMBO YA PESA:WAJUE NYOTA WA LIGI KUU ENGLAND WALIOKWENDA KUVUNA PESA CHINA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top