728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, January 03, 2016

    YANGA YAANZA KWA KISHINDO MAPINDUZI CUP YAIBAMIZA MAFUNZO 3-0

    Zanzibar

    Yanga imeanza michuano ya Mapinduzi kwa kishindo kwa kuitwanga Mafunzo kwa mabao 3-0 katika mechi ya kwanza kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar, leo.

    Mabao mawili ya Yanga yamefungwa na Donaldo Ngoma aliyepewa pasi na
    Mzimbabwe mwenzake Thabani Kamusoko katika dakika za 31 na 34 na
    kuifanya Yanga kwenda mapumziko ikiwa inaongoza kwa mabao 2-0.

    Kipindi cha pili, Mafunzo walijitutumua na kupeleka mashambulizi kadhaa
    likiwemo lililozaa penalti baada ya Kelvin Yondani kuachwa na kumvuta
    mshambuliaji wa Mafunzo, lakini kipa Deo Munishi ‘Dida’ akaipangua na baadaye kuidaka.

    Paul Nonga aliyeingia dakika 10 za mwisho kuchukua nafasi ya Tambwe alifunga bao la tatu katika dakika ya 90 huku walinzi wa Mafunzo wakiamini alikuwa ameotea.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: YANGA YAANZA KWA KISHINDO MAPINDUZI CUP YAIBAMIZA MAFUNZO 3-0 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top