728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, January 31, 2016

    AZAM FC YATAKATA ZAMBIA,YAWATOA NISHAI WAZIMBABWE SASA YAHITAJI USHINDI MMOJA TU ITWAE UBINGWA

    Ndola,Zambia.

    Klabu ya Azam FC imeendelea kuwa mwiba mkali huko Zambia katika michuano ya kimataifa inayoendelea nchi humo baada ya jana jumamosi kuilaza Chicken Inn ya Zimbabwe kwa mabao 3-1 katika mchezo mkali uliopigwa katika dimba la Levy Mwanawasa mjini Ndola.

    Azam FC imejipatia mabao hayo kupitia kwa nahodha John Bocco,Kipre Tchetche na bao la kujifunga la Brian Juru huku Nickie Muchedeyi akiifungia bao la kufutia machozi Chicken Inn.

    Kufuatia ushindi huo Azam FC itajitupa tena dimbani Februari 3 kuvaana na Zanaco FC katika mchezo wa fainali na mshindi atatangazwa bingwa wa michuano hiyo.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: AZAM FC YATAKATA ZAMBIA,YAWATOA NISHAI WAZIMBABWE SASA YAHITAJI USHINDI MMOJA TU ITWAE UBINGWA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top