728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, January 11, 2016

    MESSI MCHEZAJI BORA WA DUNIA,ATWAA BALLON D'OR KWA MARA YA TANO


    Zurich,Uswisi.

    MSHINDI!!Lionel Messi ameibuka kinara kwa mara nyingine tena baada ya leo usiku kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa dunia [Ballon d'Or] kwa mwaka 2015 huko Zurich,Uswisi.

    Messi,28 ametwaa tuzo hiyo ya tano ya dunia baada ya kupata asilimia 41.33 ya kura zote zilizopigwa huku Cristiano Ronaldo aliyeshika nafasi ya pili akiambulia asilimia 27.76 na nafasi ya tatu imekwenda kwa Neymar Jr aliyepata asilimia 7.86.

    Mbali ya Messi nyota mwingine aliyetamba usiku wa leo ni mwadada wa Kimarekani Carli Lloyd.Lloyd ameibuka kinara kwa upande wa wachezaji wa kike baada ya kutangazwa mchezaji bora wa mwaka.

    Tuzo ya kocha bora wa mwaka imeenda kwa Luis Enrique wa FC Barcelona baada ya kuwashinda Pep Guardiola na Jorge Sampaoli wa Chile.

    Jill Ellis wa Marekani ametwaa tuzo ya kocha bora wa mwaka kwa upande wa soka la wanawake.

    Kikosi:2015 FIFPro World XI

    Kipa: Manuel Neuer

    Walinzi: Thiago Silva, Marcelo, Sergio
    Ramos, Dani Alves

    Viungo: Andres Iniesta, Luka Modric, Paul Pogba.

    Washambuliaji: Neymar, Lionel Messi, Cristiano Ronaldo

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MESSI MCHEZAJI BORA WA DUNIA,ATWAA BALLON D'OR KWA MARA YA TANO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top