728x90 AdSpace

Tuesday, January 19, 2016

CHAN 2016:UGANDA,MALI HAKUNA MBABE ZATOKA SARE YA GOLI 2-2,ZAMBIA YAILAZA ZIMBABWE 1-0

Rubavu,Rwanda.


Timu ya taifa ya Uganda (The Uganda Cranes) imeanza michuano ya kombe la CHAN kwa kusuasua baada ya leo kulazimishwa sare ya kufungana magoli 2-2 na timu ya taifa ya Mali katika mchezo mkali wa kundi D uliopigwa huko Umuganda Stadium,Rubavu.

Erisa Ssekisambu na Farouk Miya waliifungia Uganda Morimakan Koïta na Hamidou Sinayoko wakifunga kwa upande wa Mali Hamidou Sinayoko.

Katika mchezo mwingine wa kundi D Zambia iliitambia Zimbabwe baada ya kuilaza kwa goli 1-0.Goli hilo lilipatikana dakika ya 57 kupitia kwa Isaac Chansa.

Michuano hiyo itaendelea tena siku ya jumatano kwa michezo ya kundi A kupigwa ambapo wenyeji Rwanda watavaana na Gabon kabla ya Ivory Coast kuvaana na.Morocco.

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: CHAN 2016:UGANDA,MALI HAKUNA MBABE ZATOKA SARE YA GOLI 2-2,ZAMBIA YAILAZA ZIMBABWE 1-0 Rating: 5 Reviewed By: Unknown