728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, January 19, 2016

    CHAN 2016:UGANDA,MALI HAKUNA MBABE ZATOKA SARE YA GOLI 2-2,ZAMBIA YAILAZA ZIMBABWE 1-0

    Rubavu,Rwanda.


    Timu ya taifa ya Uganda (The Uganda Cranes) imeanza michuano ya kombe la CHAN kwa kusuasua baada ya leo kulazimishwa sare ya kufungana magoli 2-2 na timu ya taifa ya Mali katika mchezo mkali wa kundi D uliopigwa huko Umuganda Stadium,Rubavu.

    Erisa Ssekisambu na Farouk Miya waliifungia Uganda Morimakan Koïta na Hamidou Sinayoko wakifunga kwa upande wa Mali Hamidou Sinayoko.

    Katika mchezo mwingine wa kundi D Zambia iliitambia Zimbabwe baada ya kuilaza kwa goli 1-0.Goli hilo lilipatikana dakika ya 57 kupitia kwa Isaac Chansa.

    Michuano hiyo itaendelea tena siku ya jumatano kwa michezo ya kundi A kupigwa ambapo wenyeji Rwanda watavaana na Gabon kabla ya Ivory Coast kuvaana na.Morocco.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CHAN 2016:UGANDA,MALI HAKUNA MBABE ZATOKA SARE YA GOLI 2-2,ZAMBIA YAILAZA ZIMBABWE 1-0 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top