WENYEJI
Bayern Munich wameibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya AC Milan jana
katika mchezo wa Kombe la Audi Uwanja wa Allianz Arena mjini Munich.
Kwa
ushindi huo, Bayern Munich sasa itamenyana na Real Madrid katika
fainali ya Kombe la Audi usiku wa leo, wakati AC Milan itawania nafasi
ya tatu dhidi ya Tottenham iliyofungwa na Real 2-0.
Mabao
ya Bayern Munich jana yalifungwa na Juan Bernat dakika ya 24, Mario
Gotze dakika ya 73 na Robert Lewandowski zikiwa zimesalia dakika sita.
Kiungo
mpya, Arturo Vidal aliyesajiliwa kutoka Juventus ya Italia jana
aliichezea kwa mara ya kwanza Bayern Munich Uwanja wa Allianz Arena.
Kikosi
cha Bayern Munich kilikuwa; Ulreich, Rafinha, Boateng, Lahm/Alonso
dk56, Kimmich/Alaba dk19, Hojbjerg, Rode, Bernat, Vidal,
Costa/Lewandowski dk46 na Gotze.
AC Milan; Lopez, De Sciglio, Zapata/Alex dk63, Ely, Antonelli, De Jong, Bertolacci, Bonaventura, Honda, Luiz Adriano na Bacca.
0 comments:
Post a Comment