728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 06, 2016

    KUFUZU KOMBE LA DUNIA:WACHEZAJI WA EL SALVADOR WAKATAA RUSHWA KUTOKA KWA CANADA


    Wachezaji wa timu ya taifa ya El Salvador wanasema kuwa wamekataa kuchukua hongo ili wakubali kushindwa katika mechi ya kufuzu kwa kombe la dunia dhidi ya Canada siku ya Jumanne.

    Katika mkutano na vyombo vya habari,wachezaji wa timu hiyo walicheza sauti ya mtu aliyejaribu kuwahonga kupitia kuwapatia zawadi kadhaa.Canada ni sharti iishinde El Salvador huku wakitumai kwamba Mexico itaishinda Honduras katika fainali ya mechi ya kimakundi ili kuwa na fursa ya kuendelea.

    El Salvador haiwezi kufuzu katika ya raundi ya mwisho ya kimakundi.
    ''Ni kisa kisicho cha kawaida kuweza kutokea'' ,alisema mwandishi mpekuzi wa BBC Declan Hill.
    Zawadi kuu ambayo wangepata ni dola 3,000 kwa kila mchezaji.

    Timu yote ilijitokeza na kocha wake na kusema kuwa walijaribiwa kuhongwa siku ya Jumamaosi.
    Walicheza sauti ya dakika 11 ya mtu aliyejaribu kufanya uovu huo.Hill anasema kuwa hongo hiyo ilidaiwa kutolewa na raia wa El Salvador ambaye anawajua baadhi ya wachezaji,lakini ambaye alitaka kukisaidia kikosi cha Honduras
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KUFUZU KOMBE LA DUNIA:WACHEZAJI WA EL SALVADOR WAKATAA RUSHWA KUTOKA KWA CANADA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top