728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 22, 2016

    MAN CITY BADO SUMBUFU JAMANI YAINYUKA SWANSEA CITY 2-1 KOMBE LA LIGI,KOMPANY MAJERUHI TENA


    Swansea,Wales.

    Gael Clichy (Pichani) akipongezwa na Kelechi Iheanacho na wachezaji wenzake wa Manchester City baada ya kuifungia timu hiyo bao la kwanza Uwanja wa Liberty katika ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji Swansea City kwenye mchezo wa Kombe la Ligi England usiku huu.

    Mabao ya Manchester City yalifungwa na Clichy dakika ya 49 na Aleix Garcia Serrano dakika ya 67, wakati la Swansea City lilifungwa na Gylfi Sigurdsson dakika ya 93. 



    Aidha katika mchezo huo nahodha wa Manchester City,Vincent Kompany,aliyekuwa nje kwa kipindi kirefu kutokana na majeruhi alikutana na balaa jingine baada ya kuumia tena katika mchezo wake wa kwanza baada ya miezi mitano ya matibabu.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAN CITY BADO SUMBUFU JAMANI YAINYUKA SWANSEA CITY 2-1 KOMBE LA LIGI,KOMPANY MAJERUHI TENA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top