728x90 AdSpace

Tuesday, February 16, 2016

CHELSEA YAONGEZA SURA MPYA TAYARI KUIVAA PSG LEO KATIKA LIGI YA MABINGWA ULAYA

London,England.


Kocha wa muda wa Chelsea Mdachi Guus Hiddink amelazimika kuwajumuisha makinda Matt Miazga na Jake Clarke-Salter katika kikosi cha wachezaji 20 kilichosafiri kwenda Ufaransa kuvaana na Paris Saint-
Germain katika mchezo wa kwanza wa hatua ya mtoano wa ligi ya mabingwa Ulaya huko Parc des Prince.

Hiddink amefikia uamuzi huo baada ya walinzi wake wa kati John Terry na Kurt Zouma kuwa majeruhi na hivyo kubaki na walinzi Gary Cahill pamoja na Branislav Ivanovic pekee katika nafasi hiyo. 

Mbali ya Terry na Zouma Chelsea pia itazikosa huduma za kiungo wake Nemanja Matic ambaye anakabiliwa na adhabu ya kukosa mchezo mmoja huku Oscar akitarajiwa kucheza mchezo wa leo baada ya kupona majeraha yaliyokuwa yanamkabili.

KIKOSI KAMILI
 
Makipa: Asmir Begovic, Jamal Blackman, Thibaut Courtois.

Walinzi: Cesar Azpilicueta, Gary Cahill,Jake Clarke-Salter, Branislav Ivanovic,
Matt Miazga, Baba Rahman

Viungo: Cesc Fabregas, Eden Hazard,Kenedy, Ruben Loftus-Cheek, John Mikel
Obi, Oscar, Pedro, Bertrand Traore, Willian

Mastraika: Diego Costa, Loic Remy


  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: CHELSEA YAONGEZA SURA MPYA TAYARI KUIVAA PSG LEO KATIKA LIGI YA MABINGWA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Unknown