728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, February 10, 2016

    KALOU KUITEMA IVORY COAST


    Mshambuliaji wa kimataifa ya Ivory Coast Salomon Kalou amesema anaona kuna umuhimu wa kuachana na soka la ngazi ya kimataifa.

    Mchezaji huyu wa zamani wa Chelsea ameichezea nchi yake michezo 81 na kufunga mabao 29.
    Akizungumza na Bbc kalou amesema" nimeshinda kombe la afrika nimecheza fainali mbili za kombe la dunia .Lakini nafikiri ni muda sahihi wa kuacha soka la timu ya taifa ."

    "Nitafikisha miaka 30 mwaka huu na ninaanza kufikiria kuhusu kuupumzisha mwili wangu ."
    Kalou ameongeza kwa kusema anahisi ni wakati sahihi kuelekeza nguvu zake kwenye klabu yake ya Hertha Berlin.

    Mshambuliaji huyu alijiunga na Hertha Berlin mwaka 2014 na kufunga jumla ya magoli sita katika msimu wake wa kwanza
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KALOU KUITEMA IVORY COAST Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top