728x90 AdSpace

Friday, February 12, 2016

MOURINHO KUMVUTA JOHN TERRY MAN UNITED

Manchester,England.


Mourinho atataka kufanya kazi na John Terry.Aliyekuwa kocha msaidizi wa zamani wa Chelsea Ray Wilkins amesema kuwa Jose Mourinho atataka kufanya kazi na John Terry pindi atakapopewa kazi ya kukinoa kikosi cha Manchester United msimu ujao.

Wilkins aliyewahi kuichezea Manchester United miaka ya 1979-84 amesema licha ya Terry kusema kuwa hatajiunga na klabu yoyote ya England pindi atakapoachana na Chelsea mwisho wa msimu huu lakini anaamini mapenzi ya Mourinho kwa Terry huenda yakamfanya kocha huyo Mreno kumsajili Terry ikiwa Manchester United itaamua kumpa ajira.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: MOURINHO KUMVUTA JOHN TERRY MAN UNITED Rating: 5 Reviewed By: Unknown