728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, February 15, 2016

    TFF YASIKITISHWA KUPIGWA KWA MWANDISHI



    Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa ya kupigwa kwa mwandishi wa habari za michezo wa gazeti la Mwanaspoti nchini, Mwanahiba Richard na kiungo wa timu ya Simba SC Mwiny Kazimoto mjini Shinyanga.

    Kufuatia kitendo hicho kilichotokea wakati wa mazoezi, TFF imesema tukio liliofanywa na mchezaji huyo ni kinyume na sheria, taratibu/kanuni zinazoendesha mpira wa miguu nchini, hivyo wanakilaani kitendo hicho kwa nguvu zote.

    Kwa kuwa tukio lilitokea wakati wa mazoezi, mpaka sasa TFF bado haijapokea taarifa rasmi kuhusiana na suala hilo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TFF YASIKITISHWA KUPIGWA KWA MWANDISHI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top