728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, February 27, 2016

    SASA NI YANGA NA APR KLABU BINGWA AFRIKA

    Kigali,Rwanda.

    APR ikiwa nyumbani kwenye Uwanja wa Amahoro jijini Kigali, leo imeitandika Mbabane kutoka Swaziland kwa mabao 4-0 katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, hatua ya awali.

    Kwa ushindi huo, maana yake APR imesonga mbele kwa jumla ya mabao 4-1 na sasa hakuna ubishi tena ndiyo itakayokutana na mabingwa wa Tanzania Yanga katika raundi inayofuata.

    Yanga imeishinda Cercle de Joachim ya Mauritius kwa mabao 2-0 leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 3-0 baada ya ushindi wa bao 1-0 katika mechi ya kwanza ugenini.

    Kwa upande wa APR, shukurani kubwa kwa beki wake Abdul Rwatubyaye aliyepiha hat trick katika mechi hiyo ambayo APR walionekana kutakata.

    CHANZO:SALEH JEMBE

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SASA NI YANGA NA APR KLABU BINGWA AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top