umeanzisha mfumo wa
kuwakata mishahara
wachezaji wote
watakaoshindwa kufanya
mazoezi pasipo sababu ya
msingi wala kutoa taarifa
sehemu husika, jambo
ambalo linamaanisha
inataka kila mmoja kili
yake iwepo kwa ajili ya
kuisaidia timu.
Ni wazi kuwa Simba bado
inajijenga baada ya
kupotea kimataifa katika
misimu mitatu mfululizo,
hivyo inahitaji kuwa na
wachezaji wenye ari ya
ushindi kwa timu nzima na
wenye nidhamu ya kufanya
mazoezi.
Mratibu wa klabu hiyo,
Abass Suleiman ‘Gazza’,
Ijumaa aliwaweka kikaoni
nyota wote na kuwaeleza
utaratibu huo na kuwataka
kila mmoja anapokuwa na
udhuru ni lazima atoe
taarifa sehemu husika na
kwamba siyo jukumu la
kiongozi kumuuliza
mchezaji kwa nini hajafika
mazoezini, vinginevyo
wasilaumiane mwisho wa
mwezi wakikuta akaunti zao
zinapungukiwa.
"Nilitaka kuwaweka wazi,
kila mchezaji atambue kuwa
asipokuja mazoezini,
hakuna tena kiongozi
kuanza kumtafuta mchezaji
kumuuliza sababu za
kutofika, badala yake
mchezaji ndiye atoe
taarifa kama atakuwa na
udhuru.
Tumepanga yeyote
ambaye atakosa mazoezi
pasipo taarifa sehemu
husika, wajibu wangu ni
kurekodi watoro na mwisho
wa mwezi tusije kulaumiana
akikuta amekatwa
mshahara," alisema Ally
bila kufafanua watakuwa
wakikata asilimia ngapi
kila mchezaji anapokosa
mazoezi.
0 comments:
Post a Comment