728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, June 16, 2017

    USAJILI:Pickford atua Everton na kuwa mlinda mlango ghali zaidi England

    Liverpool,England.

    MLINDA mlango kinda wa England,Jordan Pickford (Pichani) amejiunga na klabu ya Everton akitokea klabu iliyoshuka daraja ya Sunderland kwa ada ya uhamisho ya £30m.

    Pickford mwenye umri wa miaka 23 amejiunga na Everton kwa mkataba wa miaka mitano baada ya kufuzu vipimo vyake vya afya Alhamisi jioni.

    Usajili huo unamfanya Pickford kuwa mlinda mlango ghali zaidi kwa upande walinda mlango raia wa England.Pia unamfanya kuwa mlinda mlango wa tatu ghali zaidi dunia nyuma ya Ederson Moraes wa Manchester City aliyenunuliwa kwa £34.7m na Gianluigi Buffon wa Juventus aliyenunuliwa kwa £32.6m.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: USAJILI:Pickford atua Everton na kuwa mlinda mlango ghali zaidi England Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top