728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, June 09, 2017

    Hatimaye AC Milan yamnyakua Rodriguez


    Milan,Italia.

    BAADA ya tetesi za muda mrefu hatimaye klabu ya AC Milan ya Italia imefanikiwa kumsajili beki wa kushoto wa VFL Wolfsburg ya Ujerumani,Mswisi Ricardo Rodriguez. 

    Rodriguez mwenye umri wa miaka 24 ameingia mkataba wa miaka minne na AC Milan mpaka Juni 2021 baada ya VFL Wolfsburg kukubali dau la €18m.

    Rodriguez anakuwa mchezaji wa tatu kujiunga na AC Milan tangu ligi ya Seria A ilipomaliza michezo yake.Wengine ni Mateo Musacchio na Franck Kessié.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Hatimaye AC Milan yamnyakua Rodriguez Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top