728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 06, 2016

    LIGI KUU BARA:YANGA,SIMBA,AZAM FC VIWANJANI KESHO JUMATANO

    Mtwara,Tanzania.

    LIGI kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) inatarajiwa kuendelea tena kesho Jumatano kwa michezo mitatu kuchezwa katika miji ya Mtwara,Dar Es Salaam na Mbeya.

    Huko Mtwara Ndanda FC watakuwa katika uwanja wao wa nyumbani wa Nangwanda Sijaona kuwakaribisha mabingwa watetezi wa ligi hiyo,Dar Young Africans.

    Azam FC watakuwa katika dimba la Sokoine,Mbeya kuvaana na wenyeji wao Maafande wa Tanzania Prisons.

    Mabingwa wa zamani wa ligi hiyo Simba SC watakuwa katika uwanja wa Uhuru (Shamba la Bibi) Dar Es Salaam kupimana ubavu na Maafande wa Ruvu Shooting Stars.Michezo yote itaanza saa 10:00 Jioni.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LIGI KUU BARA:YANGA,SIMBA,AZAM FC VIWANJANI KESHO JUMATANO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top