728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, August 16, 2015

    ARSENAL YAONA MWEZI ENGLAND,YAIFUMUA CRYSTAL PALACE 2-1,GIROUD AFUNGUA AKAUTI YA MABAO


    London,England.

    Klabu ya Arsenal imeibuka na ushindi wa kwanza wa ligi kuu England baada ya leo kuibuka na ushindi wa bao 2-1 dhidi ya klabu ngumu ya Crystal Palace katika mchezo wa mapema uliopigwa katika dimba la Selhurst Park, jijini London.

    Arsenal ilipata bao lake la kwanza dakika ya (16) kupitia kwa straika wake Mfaransa Olivier Giroud aliyefunga kwa "Tiki Taka" akiunganisha vyema krosi ya kiungo Mesut Ozil baada ya bao hilo Crystal Palace iliamka na kufanikiwa kupata bao la kusawazisha lililofungwa na mlinzi Joel Ward dakika ya (28) ya mchezo.

    Dakika ya 55 mpira wa kichwa uliopigwa na winga Alexis Sanchez ulimgonga mlinzi wa Crystal Palace D.Delaney na kujaa wavuni na kuipatia Arsenal bao la pili na kuihakikishia pounti tatu muhimu zinazoifanya ijinasue toka mkiani mwa msimamo wa ligi kuu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ARSENAL YAONA MWEZI ENGLAND,YAIFUMUA CRYSTAL PALACE 2-1,GIROUD AFUNGUA AKAUTI YA MABAO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top