728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, September 16, 2016

    SERENGETI BOYS:TULIENI TUTAICHAPA CONGO


    Dar Es Salaam,Tanzania.

    KOCHA wa timu ya soka ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys, Bakari Shime ameahidi kuiadhibu Congo -Brazzaville katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika kwa vijana utakaofanyika keshokutwa.

    Akizungumza jana Shime alisema haangalii umri wa wapinzani wao bali anachoangalia ni uwezo wao.Alisema kuwa kikosi chake kimejiandaa vya kutosha wachezaji wake wana ari na kwamba anatarajia ushindi wa kishindo katika mchezo huo ambao watahakikisha wanatumia vyema uwanja wa nyumbani.

    Serengeti ambayo iliweka kambi ya siku 10 Shelisheli na kurejea mapema jana itashuka dimbani keshokutwa kwenye Uwanja wa Uhuru mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Afrika zitakazofanyika Madagascar mwakani.

    “Kikosi changu hakina majeruhi, kambi imetupa uzoefu mkubwa wa kupambana na vijana wa Congo-Brazzaville kwani nimewapa mbinu za kutosha na kurekebisha kasoro ambazo zilijitokeza katika mchezo wetu na Afrika Kusini."

    Alisema katika mchezo huo ingawa Serengeti ilishinda mabao 2-0 kikosi chake kilikua na upungufu hasa kwa washambuliaji wake ambao walipoteza nafasi nyingi za wazi na kwamba iwapo wangezitumia vizuri wangefunga mabao ya kutosha. Katika kambi hiyo, Serengeti ilijipima na Northern Dynamo na kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

    “Tunahitaji sapoti kutoka kwa Watanzania, sio Serengeti Boys inacheza bali Watanzania wanacheza hivyo tunahitaji sapoti kubwa katika mchezo wetu wa Jumapili dhidi ya Congo-Brazzaville,” alisema Shime.

    “Historia inaonesha mara nyingi Congo imekuwa ikitunyanyasa tukicheza nao safari hii tumejiandaa vya kutosha ili tuweze kupata matokeo mazuri katika mchezo wa nyumbani kabla ya marudiano,”alisema Shime. Serengeti inahitaji ushindi wa mabao mengi katika mchezo huo kabla ya kurudiana nchini Congo baada ya wiki mbili na mshindi atafuzu fainali hizo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SERENGETI BOYS:TULIENI TUTAICHAPA CONGO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top