728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, September 16, 2016

    TAREHE YA MANJI KUKODISHWA YANGA YAJULIKANA




    Dar Es Salaam,Tanzania.
    MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji anatarajiwa kukabidhiwa rasmi timu hiyo baada ya mchezo wao wa Ligi Kuu na Simba Oktoba Mosi mwaka huu.

    Habari zilizopatikana Dar es Salaam jana zinasema Bodi ya Wadhamini ya Yanga chini ya Fatuma Karume na Francis Kifukwe imeridhia kumkodisha rasmi Manji timu hiyo kwa miaka 10 kama alivyoomba kupitia mkutano wa dharura wa wanachama wa klabu hiyo uliofanyika Juni 11 mwaka huu kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam.

    Manji aliomba apewe klabu kwa miaka 10 na katika kipindi hicho atakuwa anachukua asilimia 75 ya mapato ya timu, huku asilimia 25 ikibaki kwa wanachama ambapo pia katika kukodishwa huko timu ya soka na nembo ya klabu zote zitakuwa chini ya kampuni zake.

    “Mkinikodisha ndani ya miaka mitatu nitahakikisha naingiza faida, na asilimia 25 ya faida itakwenda kwenye klabu, ikiwa ni hasara nitabeba mimi, na baada ya miaka 10 nitawarudishia klabu yenu muanze kununua hisa,”alisema Manji katika mkutano huo.

    Hivi karibuni Kifukwe alisema kuwa wamesharidhia kumkabidhi Manji timu na kwamba bado kuna vitu vidogo vidogo wanakamilisha.“Kimsingi tumeshakubaliana kumkodisha timu, lakini kuna marekebisho madogo madogo katika ‘Proposal’ (Mapendekezo) yake ni lazima yafanyiwe marekebisho kabla ya kumpa rasmi,” alisema. 

    Lakini hata hivyo jana mmoja wa vigogo wa klabu hiyo alithibitisha kuwa Manji atakabidhiwa timu hiyo baada ya mchezo na mahasimu wao. Hata hivyo, Kifukwe jana alipoulizwa kuhusu kumkabidhi Manji timu baada ya Oktoba Mosi alisema “Kwa upande wetu tumeshamaliza, suala hilo kwa sasa lipo mikononi mwa Kamati ya Utendaji ya Yanga, wao ndio wanapaswa kuzungumzia suala hilo”.

    Kwa upande wa Katibu wa Yanga, Baraka Deusdetit alipoulizwa kuhusiana na suala hilo alisema: “Hilo suala ni la Bodi ya Wadhamini vipi lirudi kwenye Kamati ya Utendaji, nadhani bodi ya wadhamini ndio wanapaswa kuzungumzia suala hilo, inawezekana mchakato bado haujakamilika ndio maana wanasita kuuzungumzia, ukikamilika utawekwa wazi hakuna cha kuficha,” alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TAREHE YA MANJI KUKODISHWA YANGA YAJULIKANA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top