728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, September 07, 2016

    ARSENAL YAANZA KUMSAKA MRITHI WA ARSENE WENGER




    London,Uingereza.

    Meneja wa Bournemouth,Muingereza Eddie Howe,39, ameanza kutajwa kuwa mrithi wa meneja wa Arsenal,Mfaransa Arsene Wenger,ambaye mkataba wake unaisha mwishoni mwa msimu huu.

    Kwa mujibu wa Neil Ashton wa gazeti la The Sun la Uingereza ni kwamba tayari jina la meneja huyo wa Bournemouth limeshatua kwenye meza za wakuu wa Arsenal na tayari limeshaanzwa kujadiliwa.

    Howe ambaye msimu uliopita alifanikiwa kuibakiza Bournemouth ligi kuu ameripotiwa kuwa na mvuto mkubwa ndani ya bodi ya wakuu wa Arsenal kutokana na falsafa zake pamoja na ufundishaji wake.

    Howe mwenye rekodi ya kuichezea Bournemouth michezo 270 akiwa kama mlinzi wa kutumainiwa wa klabu alistaafu kucheza soka mwaka 2007 kutokana na majeruhi.Howe amejizolea sifa kemkem kwa kuweza kuipandisha klabu hiyo kutoka daraja na pili mpaka ligi kuu.

    Arsenal imeanza kumfukuzia Howe kama tahadhari ikiwa meneja wake wa sasa Wenger,66,ataamua kutosaini mkataba mpya na kujiweka pembeni.Mpaka sasa Wenger bado hajatoa tamko kama ataendelea kusalia Arsenal ama ataondoka mwishoni mwa msimu huu pindi mkataba wake utakapokuwa umekwisha.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ARSENAL YAANZA KUMSAKA MRITHI WA ARSENE WENGER Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top