728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, September 07, 2016

    CHELSEA KWA WABRAZIL HAMUIWEZI AISEE,YAMTAKA MWINGINE JANUARI




    London,Uingereza.

    CHELSEA kwa kupenda wachezaji wa Kibrazil inaongoza aisee!!Kama ulidhani David Luiz ndiyo mchezaji wa mwisho mwenye uraia wa Brazil kujiunga na Chelsea msimu huu basi umeumia.

    Ishu iko hivi mara tu dirisha la usajili litakapofunguliwa tena mwezi Januari,Kiungo wa Santos ,Thiago Maia,19,ana asilimia kubwa za kutua Stamford Blidge.

    Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail la leo Jumatano ni kwamba Chelsea imeliweka juu kabisa  jina la Maia katika orodha ya nyota itakaowaongeza pindi dirisha la usajili la majira ya baridi la mwezi Januari litakapofunguliwa. 

    Imeripotiwa tayari Paundi Milioni 15 zimeshaandaliwa kwa ajili ya kuinasa saini ya kiungo huyo aliyeiwezesha Brazil kutwaa medali ya dhahabu ya michuano ya Olimpiki iliyofikia tamati mwezi mwezi uliopita.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CHELSEA KWA WABRAZIL HAMUIWEZI AISEE,YAMTAKA MWINGINE JANUARI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top