728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, June 11, 2017

    USAJILI:Arsenal mbioni kumnasa Golovin


    Mosco,Urusi.

    MABINGWA wa kombe la FA nchini England,Arsenal wameripotiwa kuwa mbioni kukubali kutoa kitita cha £10m ili kumsajili staa wa CSKA Moscow ya Urusi,Aleksandr Golovin.

    Matandao wa habari za michezo wa nchini Urusi wa Sports.ru umedai kuwa umepata taarifa kutoka chanzo kimoja kilicho karibu na klabu ya CSKA Moscow kuwa Arsenal iko katika hatua za mwisho mwisho kumnasa staa huyo mwenye miaka 21.

    Mtandao huo pia umeripoti kuwa baada ya kukamilika kwa usajili huo,CSKA Moscow itaomba kubaki na Golovin kwa mkopo wa msimu mmoja.

    Msimu uliopita Golovin anayetajwa kuwa na kipaji kikubwa na mwenye uwezo wa kucheza namba 11,10 na namba 8 aliichezea CSKA Moscow michezo 37 akifunga mabao matatu na kupika mengine manne.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: USAJILI:Arsenal mbioni kumnasa Golovin Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top